Joshua 18:17-21

17 aKisha ukapinda kuelekea kaskazini, ukaenda hadi En-Shemeshi na kuendelea mpaka Gelilothi, inayotazamana na Njia ya Adumimu, ukateremka hadi kwenye Jiwe la Bohani mwana wa Reubeni. 18 bUkaendelea upande wa mteremko wa kaskazini wa Beth-Araba ukateremka hadi Araba. 19 cKisha ukaenda mpaka kwenye mteremko wa kaskazini wa Beth-Hogla na kujitokeza kwenye ghuba ya kaskazini ya Bahari ya Chumvi, kwenye maingilio ya Yordani upande wa kusini. Huo ulikuwa mpaka wa kusini.
20 dNayo Yordani ikawa ndio mpaka wa upande wa mashariki.
Hii ilikuwa ndiyo mipaka iliyoonyesha urithi wa koo za Benyamini pande zote.

21 eKabila ya Benyamini, ukoo kwa ukoo, ilikuwa na miji mikubwa ifuatayo:

Yeriko, Beth-Hogla, Emeki-Kesisi,
Copyright information for SwhNEN